0
 








MBUNGE wa viti maalumu mkoani Mara kupitia vijana Ester Bulaya (CCM) amewahimiza waimbaji na watunzi wa nyimbo kutunga nyimbo za kuhimiza amani katika Taifa kutokana na kuibuka kwa matukio ambayo yanaweza kuatalisha amani na kupelekea kutokea kwa vurugu.

Kauli hiyo aliitoa juzi Mjini Bunda alipokuwa akizindua kikundi cha uimbaji wa nyimbo za Injili cha Disciples of Crist Bunda pamoja na kutambulisha album yao ya kwanza, ambacho licha ya kujishughulisha na uimbaji kinafanya kazi za utetezi wa haki za binadamu na utunzaji wa mazingira.

Alisema katika siku za hivi karibuni kumeibuka matukio ambayo yanaweza kuhatalisha amani iwapomakundi mbalimbali katika jamii hayatachukua hatua za kuelimisha namna ambavyo hatari kubwa inaweza ikatokea kutokana nakukosekana kwa amnai.

Bulaya alisema amani ni kitu muhimu muhimu katika Taifa ambapo inapokosekana inamuathiri kila mmoja hivyo hatua madhubuti zinapaswa kuchukuliwa ilikuweza kuondosha hali yoyote ambayo kwa namna moja inaweza kuhatalisha amani.

Alisema kwa sasa watu wengi katika jamii wamekuwa wakisikiliza nyimbo mbalimbali hususani za injili hivyo waimbaji na watunzi wanaweza kuitumia nafasi hiyo kufikisha ujumbe kupitia nyimbo hizo za injili ili hali hiyo isiweze kutokea katika Taifa.

"Kwanza niwashukuru kikundi cha Disciples kwa kazi kubwa mlioifanya na hii leo mnazindua kikundi chenu pamoja na album yenu ya kwanza kama wana kikundi,nyie ni watu muhimu ambao mnaweza kusisitaza amani kupitia nyimbo zenu,nawaomba mtunge nyimbo za kusisitiza jambo hilo.

"Amani inapokosekana katika Taifa ni janga ambalo litamgusa kila mmoja bila kujali nafasi yake wala kazi hivyo lazima kupitia nyimbo jamii ijue madhara ya kutokuwa na amani katika Taifa ambayo ikikosekana hakuna lolote litakalo fanyika,"alisema Bulaya.

Mbunge huyo alisema amefurahishwa na kazi zinazofanywa ka kikundi hicho ambapo licha uimbaji amedai kazi za utunzaji wa mazingira na utetezi wa haki za binadamu ni kitu muhimu  katika jamii na kuahidi kukisaidia kikundi hicho katika malengo yake waliyojiwekea.

Alisema kikundi hicho kwa kuwa kimesajiliwa kinayo nafasi ya kupata mikopo ya kuendeleza shughuli zao kwa kuwa katika mwaka huu wa fedha Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 10 kwa ajili ya vijana.

Album ya kwanza ya kikundi hicho kilichozinduliwa imebeba nyimbo za Mateso,Laiti Tungelijua,Amri ya Mungu,Moyo wa Subira,Yesu Anaweza,Yesu Mokozi,Huyu ndio Yesu na Yu Mwema ambayo tayari imeshasambazwa katika maeneo mbalimbali. 

Post a Comment